Thursday, October 18, 2018

Makabidhiano rasmi ya Ofisi ya Naibu Waziri yafanyika

Mhe. Dkt. Damas Ndubaro (Mb) Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki leo amekabidhiwa rasmi Wizara hiyo na aliyekuwa Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Suzan A. Kolimba (Mb), hafla ya makabidhiano ilifanyika katika ofisi za Wizara hiyo zilizopo Mtaa wa Makole jingo la LAPF  jijini Dodoma. Katika hafla  ya makabidhiano walihudhuria Wakuu wa Idara na Vitengo wa Wizara hiyo waliosimama nyuma ya viongozi hao.
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Ndumbaro (Mb) akimshukuru aliyekuwa Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Suzan A. Kolimba (Mb) katika hafla ya makabidhiano rasmi ya ofisi jijini Dodoma.

Picha ya pamoja ya Mhe. Dkt. Ndubaro Naibu Waziri Mambo ya Ndani na Ushirikiano wa Afrika Mashariki anayeingia katika ofisi na Mhe. Dkt. Suzan A Kolimba aliyekuwa Naibu Waziri wa Wizara hiyo anayeondoka katika ofisi hiyo wakiwa wamekaa wakibadilishana mawazo.




No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.