Friday, October 19, 2018

Dkt. Ndumbaro akutana kwa mazungumzo na Mkurugenzi wa Kamati ya CPPCC ya China

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (Mb) akisisitiza jambo wakati wa mazungumzo yake na Mkurugenzi wa Kamati ya Mambo ya Nje ya  Mashauriano ya Kisiasa ya China (CPPCC), Bw. Lou Jiwei alipofika ofisini kwake Dodoma leo tarehe 19 Oktoba, 2018 kwa lengo la kumsalimia na kumpongeza kwa kuteuliwa kushika wadhifa huo. Mkurugenzi huyo anaongoza ujumbe wa watu wanne wa Kamati hiyo ambao wapo nchini kwa mwaliko wa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Job Yustino Ndugai.

Mkurugenzi wa Kamati ya Mambo ya Nje ya Mashauriano ya Kisiasa ya China (CPPCC) Bw. Lou Jiwei akizungumza na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (Mb) walipokutana katika ofisi za Wizara hiyo zilizopo Jengo la LAPF jijini Dodoma kwa mazungumzo. Mkurugenzi huyo ni mgeni wa kwanza kutoka nchi za nje kumtembelea katika ofisi yake ya  Dodoma.

Mkurugenzi wa Kamati ya Mambo ya Nje ya Mashauriano ya Kisiasa ya China (CPPCC) Bw. Lou Jiwei akimkabidhi zawadi ya kitabu  Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (Mb) ikiwa  ni kumbukumbu ya kukutana naye  jijini Dodoma.

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (Mb) akibadilishana mawazo na Balozi wa China nchini Tanzania Mhe.  Wang Ke baada ya kumaliza mazungumzo na Mkurugenzi wa Kamati ya Mambo ya Nje ya Mashauriano ya Kisiasa ya China (CPPCC).

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.