Thursday, October 18, 2018

Dkt. Ndumbaro Akutana na Wakurugenzi na Wakuu wa Vitengo wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.


Naibu Waziri  wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (Mb) akisalimiana na Mkuu Kitengo cha Fedha na Uhasibu cha Wizara hiyo Bw. Paul Kabale  leo kabla ya kukutana na baadhi wa viongozi wa Wizara hiyo katika Ofisi zake zilizopo Mtaa wa Makole Jengo la LAPF jijini Dodoma na aliyesimama pembeni ni Bw. Mapesi Manyama  Mkurugenzi Kitengo cha Ununuzi na Ugavi.

Naibu Waziri Mhe. Dkt. Ndumbaro (Mb) akisalimiana na Bw. Japhary Kachenje Mkuu wa Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.

Mhe. Dkt. Ndumbaro (Mb.) akizungumza na baadhi ya Wakuu wa Idara na Vitengo wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,  kushoto ni Mkuu wa Kitengo cha Diaspora cha Wizara hiyo Balozi Anisa Mbega akichukua maelezo yaliyotolewa na Naibu Waziri.

Aidha baadhi ya Wakuu wa Idara na Kitengo wakimsikila Naibu Waziri Mhe. Dkt. Ndumbaro (Mb), wa kwanza kulia  Bw. Japhary Kachenje  Mkuu wa Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani, wa pili Bi. Savera Kazauru Mkurugenzi Msaidizi  Utawala na Rasilimali Watu na wa tatu  Kaimu Mkurugenzi Idara ya Marekani na Ulaya Bw. Jestus Nyamanga.

Baadhi ya Wakuu wa  Vitengo vya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakimsikiliza kwa makini Naibu Waziri Mhe. Dkt. Ndumbaro, wa kwanza kushoto Bw.  Mapesi Mnyama Mkuu wa Kitengo cha Ununuzi na Ugavi wa pili Bw.  Paul Kabale Mkuu wa Kitengo Fedha na Uhasibu na wa tatu Balozi Anisa Mbega Mkuu wa Kitengo cha Diaspora.


Picha ya pamoja ya baadhi ya viongozi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakiwa pamoja na Mhe. Dkt. Ndumbaro (Mb) Naibu Waziri wa Wizara hiyo baada ya kumaliza mazungumzo yao.





No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.