Wednesday, June 14, 2023

DKT. TAX , TIC, TTB NA ZIPA WAWASHAWISHI WAFANYABIASHARA WA AUSTRIA WAJE NCHINI


 

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Stergomena Tax akizungumza katika Mkutano na jumuiya ya Wafanyabiashara wa Austria jijini Vienna.


Kaimu Balozi na mwakilishi wa Kudumu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Umoja wa Mataifa Vienna Bi Elizabeth Rwitunga akizungumza katika Mkutano na jumuiya ya Wafanyabiashara wa Austria jijini Vienna.

Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Noel Kaganda (wa kwanza kulia) na Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Swahiba Mndeme wakifuatilia mkutano kati ya Wizara na Jumuiya ya Wafanyabiashara  Austria jijini Vienna uliofanyika tarehe 13 Juni, 2023.

Mwakilishi wa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya uwekezaji Zanzibar Bw. Khamis Dunia akizungumza katika mkutano na wafanyabiashara wa Austria uliofanyika jijini Vienna tarehe 13 Juni, 2023
Mwakilishi wa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya uwekezaji Zanzibar Bw. Khamis Dunia akizungumza katika mkutano na wafanyabiashara wa Austria uliofanyika jijini Vienna tarehe 13 Juni, 2023.

Mkurugenzi Mkuu wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania Bw. Gilead Teri akizungumza katika Mkutano na jumuiya ya Wafanyabiashara wa Austria uliofanyika jijini Vienna.

 











 

 




Waziri wa Mambo ya na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe Dkt. Stergomena Tax amekutana na kuzungumza na jumuiya ya Wafanyabiashara wa Austria jijini Vienna na kuwashawishi wafanyabiashara hao waje nchini kuwekeza, kufanya biashara na kutembelea vivutio vya utalii.

 
Dkt. Tax ameshiriki mkutano huo pamoja na Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC), Mamlaka ya Uwekezaji Zanzibar (ZIPA) na Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) ambapo kwa pamoja walielezea jinsi serikali ilivyoboresha mazingira ya kufanya biashara na uwekezaji nchini waliwashawishi kwamba Tanzania ni salama kwa mitaji yao na waje nchini pia kutembelea vivutio vya utalii


Wamewaelezea Wafanyabiashara wa Austria juu ya faida zinazoweza kupatikana kupitia uwekezaji au ubia na Serikali ya Tanzania au mtu binafsi kwamba hawatajuta kufanya hivyo.

Dkt. Tax amewahakikishia Wafanyabiashara hao kuwa Tanzania ni nchi yenye amani na usalama wake ni wa hali ya juu na hivyo ni kituo muafaka kwao kuwekeza mitaji yao na kufanya biashara na ana hakika watapata soko, faida na kurejesha fedha zao watakazowekeza nchini.


"Tanzania ni nchi yenye amani na usalama, kiufupi Tanzania ni njema na kwa hivyo mtakuwa na uhakika wa kurejesha fedha zenu mlizoweka kwa kuwa na soko la uhakika na faida pia mtapata kutokana na usalama wa mitaji yenu na kufanya biashara,” alisema Mhe. Waziri.


Akizungumza katika mkutano huo Mwakilishi wa Mamlaka ya Uwekezaji Zanzibar (ZIPA) Bw. Khamis Dunia alisema Serikali ya Mapinduzi Zanzibar imefungua milango ya uwekezaji na kuwakaribisha wenye nia ya kuwekeza Zanzibar katika maeneo ya utalii na miundombinu waje nchini kuwekeza na kujionea vivutio.


Naye Mkurugenzi Mkuu wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) amesema Serikali imeunganisha mifumo ya taasisi za usajili na uwezeshaji biashara ili kutoa huduma bora kwa wawekezaji. Taasisi hizo zinajumuisha TIC, NIDA, TRA, BRELA, Uhamiaji na Idara ya Kazi.


Naye Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) Bw. Damas Mfugale Ali waambie wafanyabiashara hao kuwa eneo la utalii lina utalii wa aina nyingi ambazo wawekezaji wanaweza kuja nchini na kutembelea maeneo hayo na kuwekeza.


Aliongeza kuwa Wafanyabiashara hao wanaweza pia kuja nchini na kuwekeza mmoja mmoja au kwa kuungana na serikali kwa njia ya ubia na hivyo kusaidia uendelezaji wa maeneo ya utalii kwa faida ya pande zote mbili.

 




No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.