Friday, June 23, 2023

DR. TAX AFANYA ZIARA CHUO CHA DIPLOMASIA INDONESIA

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax (Mb.) akiwa anaendelea na ziara yake nchini Indonesia, ametembelea Chuo Cha Diplomasia cha Indonesia.

Waziri Tax pamoja na ujumbe wake, walipokelewa chuoni hapo na Mkuu wa Chuo hicho, Bw. Mohammad Koba.

Kufuatia ziara hiyo, Tanzania na Indonesia zimekubaliana kuanzisha ushirikiano baina ya Vyuo vya Kidiplomasia, ikiwa ni pamoja na kubadilishana uzoefu katika maeneo mbalimbali ikiwemo uendeshaji wa chuo na Program za mafunzo kwa Wanadiplomasia, na kubadilishama ujuzi kwa walimu na wanafunzi wa vyuo hivyo.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax (Mb.) akisalimiana na viongozi wa Chuo Cha Diplomasia cha Indonesia baada ya kuwasili chuoni hapo kwa ziara


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax (Mb.) akizungumza na uongozi wa Chuo Cha Diplomasia cha Indonesia 
Mkuu wa Chuo cha Diplomasi cha Indonesia, Bw. Mohammad Koba akielezea historia ya chuo kwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax (hayupo pichani)

Mkuu wa Chuo cha Diplomasi cha Indonesia, Bw. Mohammad Koba akimkabidhi zawadi Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax katika picha ya pamoja na ujumbe wake pamoja na Mkuu wa Chuo cha Diplomasia Indonesia Bw. Mohammad Koba pamoja na Balozi wa Indonesia nchini Tanzania Mhe. Tri Yogo Jatmiko 

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax akimsikiliza moja kati ya wakufunzi kutoka Chuo cha Diplomasia Indonesia Bibi. Renata Siagian






No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.