Saturday, June 3, 2023

DKT. TAX AWASILI ANGOLA KUMWAKILISHA MHE. RAIS DKT SAMIA KATIKA MKUTANO WA ICGLR

 

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Stergomena Tax akisalimiana na   Waziri wa Mambo ya Nje wa Angola Mhe. Tete Antonio alipowasili katika Uwanja wa Ndege wa 4 de Fevereiro jijini Luanda, Angola kuhudhuria Mkutano wa 10 wa Dharura wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Ukanda wa Maziwa Makuu (ICGLR)


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Stergomena Tax (katikati) akizungumza na Balozi wa Heshima wa Tanzania nchini Angola Bw. Mbwana Mziray (kulia) na Mwenyekiti wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika Mhe.Moussa Faki Mahamat (kushoto) alipowasili jijini Luanda, Angola kuhudhuria Mkutano wa 10 wa Dharura wa Wakuu wa Nchi za Maziwa Makuu (ICGLR).


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Stergomena Tax akizungumza na Mjumbe Maalum wa Serikali ya Sudan Balozi Dafallah Al-Hajj wakati wa kikao cha maandalizi cha  Mkutano wa 10 wa Dharura wa Wakuu wa Nchi za Maziwa Makuu (ICGLR) utakaofanyika jijini Luanda  Angola tarehe 3 Juni 2023.


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Stergomena Tax akishiriki kikao


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Stergomena Tax (Mb.) amewasili jijini Luanda , Angola kuhudhuria Mkutano wa 10 wa Dharura wa Wakuu wa Nchi za Maziwa Makuu (ICGLR).

 
Mkutano huo utakaofanyika tarehe 03 Juni 2023 utajadili na kuangalia hali ya amani na usalama katika katika Akanda wa Maziwa Makuu hasa katika Jamhuri ya Sudan na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC).

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.