Monday, June 12, 2023

WAZIRI TAX AKUTANA NA MKURUGENZI MKUU WA UNODC JIJINI VIENNA

 


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Stergomena Tax (Mb.) akiwa na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa linalojishughulisha na udhibiti wa  biashara haramu ya dawa za kulevya na Uhalifu uliopangwa (UNODC) Mhe. Ghada Fathi Waly jijini Vienna.

 

 

 

kikao kati ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Stergomena Tax (Mb.) na. ujumbe wake na  Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa linalojishughulisha na udhibiti wa  biashara haramu ya dawa za kulevya na Uhalifu uliopangwa (UNODC) Mhe. Ghada Fathi Waly na ujumbe wake kikiendelea jijini Vienna

 


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Stergomena Tax (Mb.) amekutana na kuzungumza na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa linalojishughulisha na udhibiti wa  biashara haramu ya dawa za kulevya na Uhalifu uliopangwa (UNODC) Mhe. Ghada Fathi Waly jijini Vienna.

Mhe. Dkt. Tax ameelezea kuridhishwa kwake na kupongeza kazi zinazofanywa na Shirika hilo  kufuatia jitihada zao za kukabiliana na biashara haramu ya dawa za kulevya , ufisadi na uhalifu wa kupangwa.  

Amesema Umoja wa Mataifa na UNODC wanatekeleza jukumu muhimu katika kukabiliana na biashara haramu ya dawa, ambayo inatishia amani, usalama na afya ya watu duniani

Amesema kupitia mikakati yao kamili, mipango, na ushirikiano, wamekuwa muhimu katika kuongeza uelewa, kutoa msaada wa kiufundi na kuimarisha ushirikiano wa kimataifa ili kukabiliana na masuala yanayohusiana na dawa kwa ufanisi.


No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.