Sunday, August 25, 2024

WAZIRI CHUMI ASHIRIKI MKUTANO MAALUM WA AFYA WA TICAD 9








Naibu Waziri Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Cosato Chumi tarehe 24 Agosti 2024, ameshiriki mkutano Maalum wa afya pembezoni ya Mkutano wa Tisa wa TICAD ngazi ya Mawaziri unaofanyika jijini Tokyo. Mkutano huo uliongozwa na mada ya Ushirikiano Mpya kwa Usawa wa Afya Barani Afrika: Kuharakisha Ufikaji wa Huduma za Afya kwa Wote kwa Ubunifu kuelekea 2030.” Mkutano huo uliandaliwa na Muungano wa Chanjo (GAVI) na Tume ya Umoja wa Afrika (AUC) ulilenga kuangazia umuhimu wa ushirikiano na ubunifu katika kufanikisha upatikanaji wa huduma za afya kwa wote barani Afrika. Mkutano huo pia ulihudhuriwa na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Bunge la Japani Mhe. Fukazawa Yoichi. Kwa kushiriki katika mkutano huo Tanzania ilipata fursa ya kujionea namna bora ya kutoa huduma za afya kwa watu wote ili kuhakikisha kila Mtanzania anapata huduma hizo bila ya kikwazo cha kukosa hela.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.