Friday, August 23, 2024

NAIBU WAZIRI CHUMI AKUTANA NA NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NJE WA JAPAN

Naibu Waziri Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Cosato Chumi akisalimiana na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Japan Mhe. Kyoto Tsuji alipofika ofisini kwake jijini Tokyo kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Tisa wa ngazi ya Mawaziri wa Kimataifa wa Tokyo kuhusu Maendeleo ya Afrika utakaofanyika nchini huko tarehe 24-25 Agosti, 2024


Naibu Waziri Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Cosato Chumi akimsikiliza Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Japan Mhe. Kyoto Tsuji alipomtembelea ofisini kwake jijini Tokyo kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Tisa wa ngazi ya Mawaziri wa Kimataifa wa Tokyo kuhusu Maendeleo ya Afrika utakaofanyika nchini huko tarehe 24-25 Agosti, 2024


Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Cosato Chumi akizungumza alipomtembelea Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Japan Mhe. Kyoto Tsuji ofisini kwake jijini Tokyo. Wa kwanza kushoto ni Balozi wa Tanzania nchini Japan Mhe. Baraka Luvanda akifuatilia mazungumzo hayo


Mazungumzo yakiendelea






Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Cosato Chumi (Mb) amekutana na kuzungumza na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Japan Mhe. Kyoto Tsuji ofisini kwake jijini Tokyo.

Viongozi hao wamekubaliana kuendelea kushirikiana ili kuimarisha uhusiano na ushirikiano uliopo kati ya Tanzania na Japan kwa manufaa ya pande mbili.

 
Akizungumza katika kikao hicho Mhe. Chumi aliishukuru Serikali ya Japan kwa kuendelea kuchangia maendeleo ya Tanzania katika sekta mbalimbali ikiwemo miundombinu, uwekezaji, elimu, na afya.

Amesema Tanzania imejipanga kuhakikisha inaongeza kiwango cha biashara na uwekezaji kati yake na Japan na hivyo kuchochea ukuaji wa maendeleo ya kiuchumi na kijamii kwa manufaa ya pande zote mbili.

Naye, Mhe. Tsuji ameelezea utayari wa Japan kuendelea kushirikiana na Tanzania na kuimarisha uhusiano uliopo kwa manufaa ya nchi hizo.

Amesema Japan itaendelea kushirikiana na Tanzania na kuongeza biashara na bara la Afrika ili kuhakikisha maendeleo ya kweli yanapatikana.

Mhe. Chumia yuko nchini Japan kuhudhuria Mkutano wa Tisa wa Kimataifa wa Tokyo kuhusu Maendeleo ya Afrika (TICAD) ngazi ya Mawaziri utakaofanyika jijini Tokyo tarehe 24-25 Agosti 2024.

 

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.