Sunday, August 25, 2024

WAZIRI CHUMI ASHIRIKI UZINDUZI WA LOGO YA SUMMIT YA TICAD9 2025 JAPAN

 





Tarehe 24 Agosti,2024, Naibu Waziri Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Cosato Chumi ameshiriki katika hafla ya uzinduzi wa logo ya Mkutano wa Tisa wa TICAD wa Wakuu wa Nchi na Serikali utakaofanyika 2025 nchini Japan. 

Uzinduzi wa Logo hiyo ya Summit ya #TICAD9 umefanyika jijini Tokyo wakati wa Mkutano wa TICAD ngazi ya Mawaziri, ambao unafanya maandalizi ya Summit hiyo inayotarajiwa kufanyika tarehe 20 - 22 Agosti 2025, jijini Yokohama, Japan. Uzinduzi huo ullihudhuriwa na wadau mbalimbali kutoka sekta za umma na binafsi za nchini
Japan ambao pia, walionesha huduma mbalimbali wanazozitoa katika nchi za Afrika. 

Katika tukio hilo, Mhe. Naibu Waziri Chumi akiambatana na Balozi wa Tanzania nchini Japan Mhe. Baraka Luvanda walipata nafasi ya kusalimiana na wadau wa taasisi na kampuni za Japan zenye ubia na Tanzania.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.