Tuesday, August 13, 2024

NAIBU WAZIRI LONDO AMTEMBELEA KATIBU MKUU JUMUIYA YA AFRIKA MASHARIKI

Naibu Waziri Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki anayeshughulikia masuala ya Afrika Mashariki Mhe. Dennis Londo (Mb) akisalimiana na Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Masharki (EAC) Mhe. Monica Nduva alipomtembelea Ofisini kwake jijini Arusha.

 

Naibu Waziri Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki anayeshughulikia masuala ya Afrika Mashariki Mhe. Dennis Londo (Mb) akisaini kitabu cha wageni Ofisini kwa Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Masharki (EAC) Mhe. Monica Nduva alipomtembelea  jijini Arusha .
 

 

mazungumzo yakiendelea

Naibu Waziri Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki anayeshughulikia masuala ya Afrika Mashariki Mhe. Dennis Londo (Mb) katika picha na Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Masharki (EAC) Mhe. Monica Nduva alipomtembelea Ofisini kwake jijini Arusha.
 
 NAIBU WAZIRI LONDO AMTEMBELEA KATIBU MKUU JUMUIYA YA AFRIKA MASHARIKI


Naibu Waziri Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki anayeshughulikia masuala ya Afrika Mashariki Mhe. Dennis Londo (Mb) ametembelea Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Masharki (EAC) Mhe. Monica Nduva Ofisini kwake tarehe 13 Agosti 2024 jijini Arusha. 

Katika mazungumzo yao, Mhe. Londo alimuhakikishia Mhe. Nduva ushirikiano na kumuelezea kuwa Tanzania itashiriki katika masuala yote yanayohusu Jumuiya ya EAC kwa uzito unaostahili. 

Ziara hiyo ilikuwa na lengo la kujitambulisha na kufahamiana baada ya Mhe. Londo kuwa Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kufuatia mabadiliko madogo ya Baraza la Mawaziri yaliyofanyika mwezi Julai 2024. 

Mhe. Londo aliongozana na Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Stephen Mbundi.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.