Tuesday, August 13, 2024

WAZIRI WA MAMLAKA YA FORODHA WA CHINA AWASILI NCHINI KWA ZIARA YA KIKAZI.

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi. Said Shaibu Mussa akimpokea Waziri wa Mamlaka ya Forodha ya China, Mhe. Yu Jianhua mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, jijini Dar es Salaam.

============

Waziri wa Mamlaka ya Forodha ya China, Mhe. Yu Jianhua amewasili nchini leo Agosti 13, 2024 kwa ziara ya kikazi ya Siku tatu.

Alipowasili kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere alipokelewa na Naibu Katibu, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Said Shaib Mussa.

Ziara ya Waziri Yu Jianhua inalenga kukamilisha makubaliano yaliyofikiwa wakati wa ziara ya Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania aliyoifanya nchini China mwezi Novemba 2022.

Mhe. Waziri Yu Jianhua ndiye anahusika na kutoa vibali vya kufungua masoko ya bidhaa mbalimbali kuingia nchini China.

Akiwa nchini Tanzania, Mhe. Yu Jianhua atakutana na viongozi wa Wizara ya Maliasili na Utalii; Wizara ya Kilimo; Wizara ya Uvuvi na Mifugo; Kamishna wa TRA; na atatembelea Bandari ya Dar es Salaam.

Ujumbe wa Waziri huyo pia utatembelea Stesheni ya TAZARA ikiwa ni sehemu muhimu ya uhusiano kati ya Tanzania na China.

Itakumbukwa kwamba tayari Wizara imewezesha kupatikana soko la mihogo, soya, ufuta, kahawa, mbegu za pamba, karafuu kutoka Tanzania kuuzwa nchini China.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.