Monday, October 24, 2022

RAIS TSHISEKEDI AMALIZA ZIARA YA KITAIFA NCHINI

Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), Mhe. Felix Tshisekedi amemaliza ziara ya Kitaifa ya siku mbili aliyoifanya nchini tarehe 23 na 24 Oktoba, 2022. 

Rais. Tshisekedi ameagwa na mwenyeji wake Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan katika uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam. 

Mapema kabla ya kuondoka, Mhe. Rais Tshisekedi ametembelea mradi wa ujenzi wa Reli ya Kisasa (SGR) Jijini Dar es Salaam na kujionea hatua mradi huo ulipofikia. 

Rais Tshisekedi alipotembelea mradi wa ujenzi wa SGR, aliambatana na Waziri wa Maambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax pamoja na Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Mhe. Prof. Makame Mbarawa.

Juni 14, 2019 Rais Tshisekedi kwa mara ya kwanza alifanya ziara ya siku mbili nchini Tanzania.

Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Mhe. Felix Tshisekedi akimsikiliza Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Reli Tanzania - (TRC), Bw. Masanja Kadogosa wakati Rais Tshisekedi alipofanya ziara katika mradi wa ujenzi wa SGR Jijini Dar es Salaam. Mhe. Tshisekedi ameambatana na Waziri wa Maambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax pamoja na Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Mhe. Prof. Makame Mbarawa. 


Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Mhe. Felix Tshisekedi akimuuliza jambo Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Reli Tanzania - (TRC), Bw. Masanja Kadogosa wakati Rais Tshisekedi alipofanya ziara katika mradi wa ujenzi wa SGR Jijini Dar es Salaam

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan na Mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Kongo, Mhe. Felix Tshisekedi wakiwa katika jukwaa la salamu za heshima za kijeshi katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es salaam kabla ya Rais Tshisekedi kuondoka nchini baada ya kumaliza ziara yake

Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Mhe. Felix Tshisekedi akiagana na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es salaam baada ya kumaliza ziara yake nchini

Rais wa Jamhuri ya KIdemokrasia ya Kongo, Mhe. Felix Tshisekedi akimuaga Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es salaam baada ya kumaliza ziara yake nchini

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan pamoja na viongozi waandamizi wa serikali wakimuaga Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Mhe. FĂ©lix Tshisekedi katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam baada ya kuhitimisha ziara yake nchini





No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.