Friday, October 7, 2022

DKT. TAX AKUTANA NA BALOZI WA TANZANIA NCHINI ZAMBIA


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashriki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax (Mb.), (kulia) akiwa na Balozi wa Tanzania nchini Zambia, Mhe.  Luteni Jenerali Mathew Edward Mkingule katika Ofisi za Makao Makuu ya Wizara Mtumba, Jijini Dodoma.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashriki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax (Mb.), akizungumza na Balozi wa Tanzania nchini Zambia, Mhe.  Luteni Jenerali Mathew Edward Mkingule katika Ofisi za Makao Makuu ya Wizara Mtumba, Jijini Dodoma.

 

 

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashriki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax (Mb.), amekutana na kuzungumza na Balozi wa Tanzania nchini Zambia, Mhe.  Luteni Jenerali Mathew Edward Mkingule katika Ofisi za Makao Makuu ya Wizara Mtumba, Jijini Dodoma.

Katika kikao hicho Mhe. Mkingule alitumia nafasi hiyo kujitambulisha kwa Mhe. Waziri na kumpongeza kufuatia uteuzi alioupata hivi karibuni na kuwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki. 

Mhe. Mkingule pia alipokea maelekezo kutoka kwa Mhe. Waziri Dkt. Tax tayari kuelekea katika kituo cha kazi nchini Zambia.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.