Thursday, October 20, 2022

BALOZI CHIPETA AWASILISHA HATI ZA UTAMBULISHO KWA MFALME WA UHOLANZI

 

 

Balozi wa Tanzania nchini Uholanzi, Mhe. Caroline Kitana Chipeta akiwasilisha Hati za Utambulisho kwa Mtukufu Mfalme Willem-Alexander wa Uholanzi

Balozi wa Tanzania katika Falme ya Uholanzi, Mhe. Caroline Kitana Chipeta akizungumza na Mtukufu Mfalme Willem-Alexander wa Uholanzi baada ya kuwasilisha Hati za Utambulisho

 
Balozi wa Tanzania katika Falme ya Uholanzi, Mhe. Caroline Kitana Chipeta katika picha na Mtukufu Mfalme Willem-Alexander wa Uholanzi baada ya kuwasilisha  Hati za Utambulisho kwa Mfalme huyo

Balozi wa Tanzania  katika Falme ya Uholanzi, Mhe. Caroline Kitana Chipeta katika picha ya pamoja na maafisa Ubalozi wa Tanzania nchini humo baada ya kuwasilisha  Hati za Utambulisho kwa Mfalme wa Uholanzi

Balozi wa Tanzania nchini Uholanzi, Mhe. Caroline Kitana Chipeta alipowasili katika kasri  lililoko Noordeinde, The Hague,  Uholanzi kuwasilisha Hati za Utambulisho kwa Mtukufu Mfalme Willem-Alexander wa Uholanzi 


 

Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Falme ya Uholanzi , Mhe. Caroline Kitana Chipeta, awasilisha Hati za Utambulisho kwa Mtukufu Mfalme Willem-Alexander wa Uholanzi.

 

Hafla hiyo imefanyika katika moja ya Kasri za Kifalme iliyoko Noordeinde, The Hague,  Uholanzi tarehe 19 Oktoba, 2022.

 

Julai 2022, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan alimteua Balozi Caroline Kitana Chipeta kuwa Balozi wa Tanzania katika Falme ya Uholanzi.


No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.