Monday, October 10, 2022

RAIS DKT. RUTO ALIPOWASILI IKULU DAR ES SALAAM


Rais wa Jamhuri ya Kenya Mhe. Dkt. William Samoei Ruto akiwasili Ikulu jijini Dar es Salaam na kupokelewa na mwenyeji wake Rais wa Jamhuri ya Muungno Mhe. Samia Suluhu Hassan.

Rais wa Jamhuri ya Muungano Mhe. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Rais wa Jamhuri ya Kenya Mhe. Dkt. William Samoei Ruto alipowasili Ikulu jijini Dar es Salaam

Rais wa Jamhuri ya Kenya Mhe. Dkt. William Samoei Ruto akisalimiana na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kasim Majaliwa alipowasili Ikulu jijini Dar es Salaam na kushuhudiwa na mwenyeji wake Rais wa Jamhuri ya Muungano Mhe. Samia Suluhu Hassan.

Rais wa Jamhuri ya Kenya Mhe. Dkt. William Samoei Ruto akisalimiana na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Katiba Sheria, Utumishi na Utawala Bora Zanzibar, Mhe Haroun Ali Suleiman alipowasili Ikulu jijini Dar es Salaam na kushuhudiwa na mwenyeji wake Rais wa Jamhuri ya Muungano Mhe. Samia Suluhu Hassan.

Rais wa Jamhuri ya Kenya Mhe. Dkt. William Samoei Ruto akisalimiana na Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Joseph Sokoine alipowasili Ikulu jijini Dar es Salaam na kushuhudiwa na mwenyeji wake Rais wa Jamhuri ya Muungano Mhe. Samia Suluhu Hassan.

Rais wa Jamhuri ya Kenya Mhe. Dkt. William Samoei Ruto akisalimiana na Balozi wa Tanzania nchini Kenya Mhe. Dkt. John Simbachawene  alipowasili Ikulu jijini Dar es Salaam na kushuhudiwa na mwenyeji wake Rais wa Jamhuri ya Muungano Mhe. Samia Suluhu Hassan.

Rais wa Jamhuri ya Kenya Mhe. Dkt. William Samoei Ruto akisalimiana na Mkurugenzi wa Idara ya Afrika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Naimi Azizi alipowasili Ikulu jijini Dar es Salaam na kushuhudiwa na mwenyeji wake Rais wa Jamhuri ya Muungano Mhe. Samia Suluhu Hassan.


 

 

 

 

 

Rais wa Jamhuri ya Kenya Mhe. Dkt. William Samoei Ruto amewasili Ikulu jijini Dar es Salaam na kupokelewa na mwenyeji wake Rais wa Jamhuri ya Muungano Mhe. Samia Suluhu Hassan.

Mhe. Dkt. Ruto na mke wake Mama Rachel Ruto wako nchini kwa ziara ya kikazi ya Siku mbili waliwasili nchini tarehe 09/10/2022 na kupokelewa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Stergomena Tax katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, jijini Dar es Salaam.

Akiwa Ikulu Mhe. Dkt. Ruto alifanya mazungumzo ya faragha na mwenyeji wake Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan na baadaye walikuwa na mazungumzo rasmi ambayo yalihudhuriwa na wajumbe wa pande zote mbili.

Viongozi hao walipomaliza mazungumzo yao walikutana na waandishi wa habari na kuzungumzia walichojadili kwa umoja wao.

Baadaye viongozi hao walielekea katika ukumbi maalum ambako Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan aliandaa dhifa malum kwa ajili ya mgeni wake Mhe. Rais Ruto.

Baada ya dhifa hiyo Mhe. Rais Ruto na ujumbe wake waliondoka nchini kurejea Kenya.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.