Wednesday, March 13, 2019

Balozi wa Canada atembelea Wizara ya Mambo ya Nje

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Balozi wa Canada atembelea Wizara ya Mambo ya Nje 

Bw. Jestas A. Nyamanga, Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika-Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki amekutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Canada hapa nchini Mhe. Pamela O’Donnell tarehe 11 Machi 2019.

Mazungumzo hayo yaliyofanyika jijini Dar es Salam yamelenga kuimarisha uhusiano baina ya Tanzania na Canada. Mataifa haya mawili, kwa kipindi kirefu yamekuwa yakishirikiana kwenye masuala ya afya, elimu, ukuzaji wa uchumi, Utawala Bora pamoja na biashara na uwekezaji.

Katika mazungumzo hayo, Balozi wa Canada amemhakikishia Kaimu Mkurugenzi kuwa, Serikali ya Canada inaendelea kuunga mkono jitihada za Serikali ya awamu ya tano katika kuleta Maendeleo na kuondoa umaskini na kwamba Canada itatekeleza kwa ufanisi miradi iliyopo inayotekelezwa kupitia Serikali , Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Asasi zisizo za Kiserikali(NGOs).

Wakati huo huo, Kaimu Mkurugenzi alimkaribisha Balozi huyo mpya nchini na kuishukuru Serikali ya Canada kwa ushirikiano mzuri na wakihistoria uliodumu baina ya Tanzania na Canada .

Aidha, aliishukuru Serikali ya Canada kwa kuisaidia Tanzania katika miradi muhimu na ya kipaumbele hususan miradi ya afya, elimu na ukuzaji wa uchumi. Alimhakikishia ushirikiano thabiti wa Wizara na Serikali kwa jumla katika kuhakikisha miradi iliyopo inatekelezwa kwa ufanisi na mingine mipya inaibuliwa.
Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,
Dodoma.
13 Machi 2019

Bw. Jestas A. Nyamanga, Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika akimkaribisha Balozi wa Canada hapa nchini Mhe. Pamela O’ Donnell

Bw. Jestas A. Nyamanga, Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika-Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki amekutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Canada hapa nchini Mhe. Pamela O’Donnell.


Bw. Jestas A. Nyamanga, Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika akiendelea kufanya majadiliano na Balozi wa Canada hapa nchini Mhe. Pamela O’ Donnell.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.