Tuesday, March 26, 2019

Mtanzania ateuliwa kuongoza Taasisi ya Kimataifa nchini China

Balozi Ali Mchumo

=============================================================
Balozi Mstaafu, Mhe. Ali Mchumo (Pichani) kutoka Tanzania ameteuliwa kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kimataifa ya International Network for Bamboo and Rattan (INBAR) yenye makao yake makuu mjini Beijing, China. Taarifa ya uteuzi wake imetangazwa tarehe 25 Machi 2019 katika tovuti ya taasisi ya INBAR. Taasisi ya INBAR ilianzishwa mwaka 1997 kwa madhumuni ya kukuza matumizi ya mianzi (Bamboo) kama njia endelevu ya utunzaji wa mazingira . Taasisi hiyo inaundwa na nchi wanachama 45 na ina ofisi zake za kanda nchini  Ethiopia, Ghana na Equador. Tanzania ni mojawapo ya nchi mwanachama mwanzilishi wa taasisi hiyo na imenufaika na uwepo wa taasisi hiyo kupitia miradi mbalimbali iliyofadhiliwa na INBAR pamoja na mafunzo kwa wataalam wa zao la mianzi. 


No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.