Tuesday, March 26, 2019

Balozi wa Tanzania nchini Sudan akutana na Mkuu wa Chuo Kikuu cha Kimataifa cha Afrika

Balozi wa Tanzania nchini Sudan, Mhe. Silima Kombo Haji,  amekutana na kufanya  mazungumzo rasmi na Mkuu wa Chuo Kikuu cha Kimataifa cha Afrika (International University of Africa - IUA), Profesa Kamal Muhammed Ubeid, mjini Khartoum, Sudan. Katika mazungumzo baina yao, Prof. Ubeid alimhakikishia Balozi Silima kuwa, chuo hicho kitaendeleza ushirikiano  na Tanzania kwa kuendelea kutoa ufadhili wa elimu ya juu kwa wanafunzi wengi zaidi wa Kitanzania kadri hali itakavyoruhusu.
Takribani wanafunzi wa Kitanzania wapatao 517 wanaosoma katika vyuo mbalimbali nchini Sudan ambapo 490 kati yao wanasoma katika chuo hicho kilichopo Khartoum katika fani mbalimbali zikiwemo uhandisi wa mafuta na gesi, uchumi, udaktari na dawa na maabara, sheria, lugha na fani nyinginezo. 


Balozi Silima mara baada ya mazungumzo na Profesa Ubeid.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.