Tuesday, March 19, 2019

Naibu Katibu Mkuu afungua mkutano kati ya Wabunge wa EALA na wadau kuhusu kilimo

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Ramadhan Muombwa Mwinyi akifungua mkutano wa Kamati ya Kilimo, Utalii na Maliasili ya Bunge la Jumuiya ya Afrika Mashariki (EALA) ambayo inakusanya maoni kutoka kwa wadau mbalimbali kuhusu namna ya kuboresha bajeti katika sekta ya Kilimo kwenye nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki mpaka kufikia asilimia 10. Mkutano huo umehudhuriwa na Wabunge wa Bunge hilo kutoka nchi wanachama. Ufunguzi wa mkutano  huo umefanyika katika Hotel ya Mt. Gasper iliyopo jijini Dodoma tarehe 19 Machi 2019.
Sehemu ya Wabunge wa Bunge la Jumuiya ya Afrika Mashariki wakifuatilia hotuba ya ufunguzi wa mkutano huo. Kutoka kushoto ni Mhe. Adam Omari Kimbisa, Mhe. Dkt. Oburu Oginga na  Mhe. Nooru Adan Mohammed 
Juu na Chini ni sehemu ya wadau mbalimbali waliohudhuria Mkutano huo.




Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Sera na Mipango katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Joachim Otaru naye akifuatilia ufunguzi wa mkutano huo
Balozi Mwinyi akiendelea kuzungumza katika ufunguzi wa Mkutano huo.
Wajumbe wengine wakifuatilia ufunguzi wa mkutano huo. Kushoto ni Mhe.Mhandisi Mohammed H. Mnyaa.

Mhe. Ramadhan Muombwa Mwinyi akiwa katika picha ya pamoja na Kamati ya Kilimo, Utalii na Maliasili ya Bunge la Jumuiya ya Afrika Mashariki pamoja na wadau kutoka sekta na taasisi mbalimbali waliohudhuria mkutano kuhusu namna ya kuboresha bajeti katika sekta ya kilimo kwenye nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.   









No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.