Thursday, March 21, 2019

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Mambo ya Nje wa Qatar aitembelea Tanzania




Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Mambo ya Nje wa Qatar, Mhe. Mohammed Bin Abdulrahman Al-Thani, amewasili  nchini na kupokelewa na Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Faraji Kasidi Mnyepe, jana tarehe 20 Machi, 2019. Mhe. Al-Thani atakuwa nchini kwa siku moja ambapo atakutana na kufanya mazungumzo na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli, kabla ya kuondoka kuelekea Rwanda.


Sehemu ya ugeni huo ukiwasili.
Wajumbe wa msafara huo wakisalimiana na viongozi wa serikali waliofika katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, kuwapokea akiwemo Balozi wa Tanzania nchini Qatar  Mhe. Fatma Mohammed Rajab na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Ayoub Mndeme.

Mmoja kati ya maafisa wa msafara huo akisalimiana na afisa wa Ubalozi wa Qatar nchini.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.