Thursday, March 28, 2019

Fursa za ajira.


TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

NAFASI ZA AJIRA KATIKA SEKRETARIETI YA JUMUIYA YA MADOLA, LONDON, UINGEREZA.

Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, inawahimiza Watanzania wenye sifa kuomba nafasi za ajira katika Sekretarieti ya Jumuiya ya Madola, London, Uingereza.

Ajira hizo ni kama ifuatavyo:-

1.           Mshauri wa masuala ya Miundombinu na Usanifu wa Majengo        (Advisor Infrustructure and Architecture);
2.           Mkurugenzi wa masuala ya Uchumi, Vijana na Maendeleo      Endelevu (Senior Director, Economic, Youth and Sustainable         Development) na
3.           Mshauri  na Mkuu wa Kitengo cha Biashara na Ushindani (Advisor and Head,   Trade and Competitiveness section).

Watanzania wenye sifa wanahamasishwa kuomba nafasi hizo hasa ikizingatiwa kuwa, nchi wanachama wa Jumuiya ya Madola ambazo hazina watumishi wengi katika ngazi ya maafisa waandamzi watapewa  kipaumbele ili kuimarisha uwiano wa kikanda katika nafasi hizo za ajira.
Kwa kuzingatia sera ya Jumuiya ya Madola ya usawa wa kijinsia, Sekretarieti ya taasisi  inawahimiza wanawake wengi zaidi wenye vigezo kuomba nafasi hizo.
Taarifa zote muhimu kuhusu fursa hizo za ajira zinapatikana kwa kupitia tovuti http://thecommonwealth.org.jobs.
Mwisho wa kutuma maombi kwa nafasi hizo ni tarehe 10 Aprili, 2019; tarehe 16 Aprili, 2019 na tarehe 17 Aprili, 2019, mtawalia.

 Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,
Dodoma
28 Machi, 2019.



No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.