Saturday, March 23, 2019

Waziri wa Mambo ya Nje azungumza na Watumishi wa Wizara

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi akipokelewa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mahsariki, Dkt. Faraji Kasidi Mnyepe mara baada ya kuwasili kwenye eneo la Ukumbi wa Mikutano la Informatics lililopo Chuo Kikuu cha Dodoma kwa ajili ya kukutana kwa mara ya kwanza na Watumishi wa Wizara tarehe 23 Machi 2019
Mhe. Prof. Kabudi akizungumza na Watumishi wa Wizara (hawapo pichani) alipokutana nao kwa mara ya kwanza  baada ya kuteuliwa na Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwenye nafasi hiyo tarehe 3 Machi 2019. Pamoja na mambo mengine, Mhe. Prof. Kabudi aliwataka Watumishi wa Wizara kubadilika na kutekeleza majukumu yao kwa kuzingatia sheria, kanuni, taratibu miongozo na maelekezo mbalimbali pamoja na kuwa wazalendo na kufanya kazi zao kwa kushirikiana na  kwa weledi ili kufikia malengo yaliyokusudiwa.


Sehemu ya Watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakimsikiliza Mhe. Prof. Kabudi ambaye haonekani pichani alipozungumza nao


Sehemu nyingine ya Watumishi wakifurahia jambo wakati wakimsikiliza Mhe. Prof. Kabudi (hayupo pichani)


Watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakiwa kwenye mkutano wao na Mhe. Waziri


Mkutano ukiendelea huku Watumishi wa Wizara wakifuatilia

Sehemu nyingine ya Watumishi


Mhe. Prof. Kabudi alitumia fursa ya mkutano wake na Watumishi wa Wizara kugawa Ilani ya Chama cha Mapinduzi ya mwaka 2015 kwa Wakuu wa Idara na Vitengo wa Wizara na kuwaagiza kuitekeleza kwani ni miongoni mwa miongozo muhimu katika utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku. Pichani Mhe. Waziri akimkabidhi Mkurugenzi wa Ofisi ya Mambo ya Nje Zanzibar, Balozi Mohammed Hamza Ilani hiyo
Mhe. Waziri akimkabidhi Mkurugenzi wa Idara ya Siasa, Ulinzi na Usalama Ilani ya Chama cha Mapinduzi
Mhe. Prof. Kabudi akimkabidhi Ilani ya Chama cha Mapinduzi Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Sera na Mipango, Bw. Joachim Otaru
Mhe. Prof. Kabudi akimkabidhi Ilani ya Chama cha Mapinduzi, Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Afrika, Bw. Wilbroad Kayombo
Mkurugenzi wa Idara ya Siasa, Ulinzi na Usalama akitoa neno la shukrani kwa niaba ya Watumishi na kuahidi kutekeleza maelekezo yote yaliyotolewa na Mhe. Waziri
Mhe. Waziri (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wa meza kuu. Kulia kwake ni Katibu Mkuu, Dkt. Mnyepe na kushoto kwake ni Naibu Katibu Mkuu, Balozi Ramadhan Muombwa Mwinyi. Kushoto ni Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Usimamizzi wa Rasilimali Watu, Bibi Savera Kazaura na kulia ni Bw. Hassan Mnondwa, Mwenyekiti wa TUGHE Wizarani .

Mhe. Prof. Kabudi akiwa katika picha ya pamoja na Wakuu wa Idara na Vitengo


No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.