Friday, March 22, 2019

Prof. Kabudi awasilisha taarifa ya utekelezaji wa bajeti ya Wizara kwa Kamati ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb.) akiwasilisha Taarifa ya utekelezaji wa bajeti ya Wizara kwa mwaka wa fedha 2018/2019 na Taarifa kuhusu makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara kwa mwaka wa fedha 2019/2020 mbele ya Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama (NUU) (hawapo pichani) wakati wa kikao kati ya Kamati hiyo na Wizara kilichofanyika kwenye Ofisi za Bunge, Dodoma tarehe 22 Machi, 2019. Kulia ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Faraji Kasidi Mnyepe na kushoto ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki  Balozi Ramadhan M. Mwinyi.
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama (NUU), Mhe. Mussa Azan Zungu akimsikiliza Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb.) (hayupo pichani), wakati akiwasilisha taarifa kuhusu bajeti ya Wizara yake wakati wa kikao kati ya Kamati hiyo na Wizara kilichofanyika Ofisi za Bunge, Dodoma tarehe 22 Machi, 2019. Wakati wa kikao hicho, Mhe. Zungu alitumia fursa hiyo kwa niaba ya Kamati, kumpongeza Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa hatua ya kupeleka haraka misaada ya chakula na dawa kwa nchi za Malawi, Msumbiji na Zimbabwe baada ya kupatwa na maafa  yaliyosababishwa na kimbunga kikali kilichozikumba nchi hizo.
Kikao kati ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama na Wizara ya mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kikiendelea
Sehemu ya Wabunge ambao ni Wajumbe wa Kamati hiyo wakifuatilia kikao
Sehemu ya Wakurugenzi kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakiwa kwenye kikao na Kamati ya Bunge ya NUU
Wajumbe wa Kamati wakimsikiliza Mhe. Waziri (hayupo pichani)
Wakuu wa Idara na Vitengo kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakifuatilia kikao
Mjumbe wa Kamati akichangia hoja wakati wa kikao hicho
Sehemu nyingine ya Wakuu wa Idara na Vitengo wa Wizara wakiwa kwenye kikao na Kamati ya Bunge ya NUU
Mjumbe wa Kamati akichangia jambo wakati wa kikao na Wizara
Mjumbe mwingine wa Kamati ya Bunge ya NUU akichangia hoja wakati wa kikao kati ya Kamati hiyo na Wizara
Mhe. Mbunge akichangia hoja 

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.