Sunday, March 17, 2019

Waziri Kabudi awashukuru wajumbe wa wizara mbalimbali walioshiriki katika mkutano wa Baraza la Mawaziri la SADC.

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Faraji Kasidi Mnyepe, akifungua kikao baina ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi(Mb.), na wajumbe wa wizara mbalimbali walioshiriki katika Mkutano wa Baraza la Mawaziri la Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC Council of Ministers).
Mhe. Kabudi ametumia kikao hicho kuwashukuru wajumbe wa wizara mbalimbaliza serikali zilizoshiriki katika mkutano huo kwa umakini ambao wameuonesha.

Mheshimiwa Kabudi akisisitiza jambo wakati wa mkutano huo.Kushoto kwake ni Waziri wa Viwanda na  Biashara, Mhe. George Kakunda (Mb.); na kulia kwake ni Waziri Ofisi ya Rais, Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Mhe. Issa Haji Ussi Gavu.

Makatibu wakuu na wajumbe walioshiriki katika kikao hicho.

Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kikanda ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Bibi. Agnes Kayola akifuatilia mkutano huo.

Mkutano unaendelea

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.