Friday, March 8, 2019

Sakata la Chuo cha Diplomasia lahamia Takukuru

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Faraji K. Mnyepe (kulia) akikabidhi ripoti za ukaguzi za Chuo cha Diplomasia, kwa Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa nchini (PCCB), Bw. Diwani Athumani kwa ajili ya kufanya uchunguzi wa tuhuma za ubadhilifu wa fedha uliofanywa na baadhi ya viongozi wa chuo hicho. Makabidhiano hayo yalifanyika leo kwenye Ofisi ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki jijini Dar Es Salaam.
Mwenyekiti wa Bodi ya Chuo cha Diplomasia, Balozi Ombeni Sefue akishuhudia makabidhiano ya ripoti za ukaguzi ambazo zimeainisha ubadhilifu wa fedha katika Chuo cha Diplomasia.
Balozi Sefue (kushoto), Dkt. Mnyepe na Bw. Diwani wakibadilishana mawazo kuhusu utendaji kazi wa Chuo cha Diplomasia. 
Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU, Bw. Diwani Athumani akiagana na Mwenyekiti wa Bodi ya Chuo cha Diplomasia, Balozi Ombeni Sefue.




No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.