Wednesday, March 20, 2019

TANZANIA YANGA’RA KWENYE MASHINDANO YA SPECIAL OLYMPICS, ABU DHABI, UAE.

Mhe. Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk, Balozi wa Tanzania UAE akiongozana na Bw. Timothy Shriver, Mwenyekiti wa Special Olympics International, wakiingia uwanja wa Sheikh Zayed Sports City kwenye ufunguzi wa Special Olympics pamoja na timu ya Tanzania walioshiriki Special Olympics Internationalyaliyofunguliwa rasmi tarehe 14 Machi 2019 na Mtukufu Sheikh Mohamed bin Zayed Al Nahyan, Mrithi wa Mtawala wa Abu Dhabi na Naibu Amri Jeshi Mkuu wa Vikosi vya Ulinzi UAE.
Bonaventura Francis Anga ameshinda mbio za mita 3,000. na kupata medali ya dhabu, kwenye mashindano ya Special Olympics, Dubai.
Khalifani Ally Jihadi alishiriki mbio za mita 200 na ameshinda medali ya dhabu kwenye mashindano ya Special Olympics, Dubai.







Uzinduzi wa mashindano ya watu wenye ulemavu wa akili (Intellectual Disability) ulifanyika Abu Dhabi tarehe 14 Machi 2019 na Mtukufu Sheikh Mohamed , Mrithi wa Abu Dhabi na Naibu Amri Jeshi Mkuu wa Vikosi vya Ulinzi, UAE. Mashindano hayo yataendelea mpaka tarehe 21 Machi 2019.  Nchi 183 zinashiriki kwenye Special Olympics.

Timu ya Tanzania wanashiriki, ikiwemo wanamichezo 15 na viongozi, na makocha pamoja na walenzi 13 Tanzania imewakilishwa na timu mbili, moja ya riadha ipo Dubai wenye wanamichezo 6, na timu ya mpira wa wavu ipo Abu Dhabi yenye wachezaji 9.

Timu ya Tanzania inaendelea kufanya vizuri katika riadha.  Wanamichezo wameweza kupata jumla ya medali 3 za dhabu, kwenye mbio za mita 200, 400, na 3000, medali ya fedha 1 na 2 za shaba.

Timu ya Tanzania ya mpira wavu imefuzu kucheza fainali kesho itakayofanyika kesho tareh 20 Machi 2019 baada ya kuifunga Marekani (USA) kwa seti 2 kwa sifuri.  Fainali kwsho ni kati ya Tanzania na Italia kwa ajili ya medal ya dhahabu au fedha.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.