Tuesday, March 19, 2019

Tanzania yapeleka msaada wa chakula na madawa kwa nchi za Malawi, Msumbiji na Zimbabwe kutokana na kukumbwa na mafuriko


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba Kabudi na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto,  Mhe. Ummy Mwalimu wakiwa na Balozi wa Malawi, Mhe. Glad Chembe Munthali (kushoto), Balozi wa Msumbiji, Mhe. Monica D.C. Mussa (wa pili kushoto) na Balozi Mdogo wa Zimambwe nchini, Mhe. Martin Tavenyika (wa tatu kushoto) wakati wa zoezi la kuwakabidhi  mabalozi hao  misaada ya dawa na chakula ambavyo Serikali ya Tanzania imetoa kwa nchi zao ambazo zimekumbwa na maafa yaliyosababishwa na mafuriko kufuatia tufani kali iliyolikumba eneo hilo la kusini mwa Afrika. Tukio hilo limefanyika kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam tarehe 19 Machi 2019

Mhe. Prof. Kabudi akisikiliza maelezo kutoka kwa Mhe. Waziri Ummy kuhusu aina ya dawa zilizotolewa msaada kwenye nchi za Malawi, Msumbiji na Zimbabwe kufuatia maafa yaliyosababishwa na mafuriko yaliyozikumba nchi hizo
Add caption
Sehemu ya magari yaliyobeba shehena ya msaada wa dawa na chakula kwa ajili ya waathirika wa mafuriko kwenye nchi za Malawi, Msumbiji na Zimbabwe kama inavyoonekana kabla ya kuanza kupakiwa kwenye ndege
Askari wa Jeshi la Ulinzi wakishusha kwenye magari na kupakia kwenye ndege misaada ya madawa na chakula ambavyo Serikali ya Tanzania imetoa msaada kwa nchi za Malawi, Msumbiji na Zimbabwe  ambazo zimekumbwa na maafa ya mafuriko kufuatia tufani kali iliyolikumba eneo hilo la kusini mwa Afrika
Askari hao wakiwajibika
Mhe. Prof. Kabudi akiwa ameongozana na Mhe. Waziri Ummy , Mabalozi na Viongozi mbalimbali mara baada ya kukamilisha zoezi la kuwakabidhi Mabalozi  misaada ya dawa na chakula vilivyotolewa na Serikali ya Tanzania kwa ajili ya nchi zao zilizopatwa na maafa yaliyosababishwa na mafuriko kufuatia tufani kali iliyozikumba baadhi ya nchi za Kusini mwa Afrika. Kulia ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Faraji Kasidi Mnyepe.
Picha ya pamoja


Mhe. Prof. Kabudi akiagana na Balozi wa Msumbiji nchini, Mhe. Monica mara baada ya kukabidhi misaada kwa nchi zao

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Mnyepe naye akiagana na Mhe. Balozi Monica

Brigedia Jenerali Francis Shirima  wa kikosi cha anga cha Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) akizungumza na waandishi wa habari baada ya kukabidhiwa jukumu la  kuipeleka misaada ya dawa na chakula katika nchi za Malawi, Msumbiji na Zimbabwe  ambazo zimekumbwa na maafa yaliyosababishwa na mafuriko kufuatia tufani kali iliyolikumba eneo la kusini mwa Afrika



No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.